TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, June 27, 2015

Bendi ya Them Mushrooms kutua Dar es Salaam!!!!

Wasanii wa Them Mushrooms
Kuna tetesi zinazodai kuwa bendi ya Them Mushrooms ya jijini Nairobi inatalajiwa kutua jijini Dar kushiliki kwenye tamasha la COAST NITE linalotalajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza hapa Tanzania mwezi wa nane.

Tamasha hilo ufanyika mara mbili kila mwaka jijini Nairobi kwa kuzishilikisha bendi za taarab toka hapa nchini Tanzani.

Bendi zilizo wahi kushiriki kwenye tamasha hilo ni New Zanzibar star, The East African Melody, TOT taarab, Mashauzi na Dar Modern.
Kwa mwaka huu jijini Nairobi tamasha hilo litafanyika ijumaa ya tar 6 mwezi wa kumi (06/10/2015) na moja na bendi itakayo kwenda itajulikana mwezi ujao wa saba.


Coast Nite ni tamasha lililo sajiliwa Nairobi na sasa tunalisajili Tanzania hivyo litakua linafanyika Nairobi na Dar kila mwaka Lengo letu ni ifikapo 2017 iwepo Afika Mashariki nzima Kenya, Tanzania, Rwanda, Burundi na Uganda kwani kote huko mazungumzo yanaendelea vizuri. Mmoja wa waandaaji wa Tamasha hilo aliimegea Blog hii ya Taarabuzetu.blogspot.com 

Thursday, June 25, 2015

Je!, Waijua Bendi ya Them Mushrooms ya Nchini Kenya....?????



Them Mashurooms,
Bend ya nchini Kenya ni moja ya bend maalufu afrika mashariki iliyo dumu kwa zaidi ya miaka 40 na imejipatia umaalufu mkubwa barani ulaya kwa ushiliki wao katika maonyesho mbali mbali barani humo.



Pamoja na kua na umri mkubwa lakini bendi hiyo bado ipo imara kama chuma cha reli.
Bendi zilizo wahi kushiliki tamasha la "Coast nite" mjini nairobi toka Tanzania ni New Zanzibar star, Melody, TOT Taarab, Mashauzi na Dar modern.

Baadhi ya picha wakiwa kwenye matamasha hizi hapa:-







Kwa habari zaidi juu ya Them Mushrooms Band utaendelea kuzipata hapa...

Karibu sana.

Saturday, June 13, 2015

Mfalme Mzee Yusuph kutangaza nia kuwania ...

Mfalme wa Taarab Mzee Yusuph, Mkurugenzi wa Jahazi
Mkurugenzi wa Jahazi Modern Taarab Mfalme wa Taarab Mzee Yusuph siku ya Jumamosi ya tarehe 13/06/ 2015 katika onesho lake pale Travertine Magomeni atatangaza nia.

Mzee yusuph ambaye ni Muimbaji na Mpiga kinanda mahili ameidokezi blog hii ya Taarabuzetu.blogspot.com kuwa, siku hiyo atatangaza nia yake ya kugombea ..... katika kinyang'anyilo kinachokuja. Mmeamua kujitosa kwa kuona kuwa anafaa ila kaahidi kuzungumza mengi zaidi mbele ya mashabiki.

Usikose siku hiyo kumsapoti Mfalme Mzee Yusuph...

Saturday, June 6, 2015

UZINDUZI WA #OGOPA KOPA'Z WASOGEZWA MBELE"...

Malkia Khadija omary kopa
ULE uzinduzi wa kundi jipya la mipasho Tanzania, #Ogopa kopa'z uliyokuwa ufanyike Juni 13 mwaka huu 2015, ndani ya #Escape One, jijini Dar es salaam, umesogezwa mbele ili kuupisha mwezi mtukufu wa #Ramadhan.

Mkurugenzi wa kundi hilo, Malkia Khadija omary kopa alisema jijini Dar es salaam jana akiueleza mtandao huu wa taarabuzetu.blogspot.com kuwa, Uongozi wa juu ndani ya kundi lake ulifikiria makubaliano ya kuusogeza mbele uzinduzi huo:-
"Tunaomba radhi mashabiki wetu na tunaahidi kutangaza tarehe nyingine ya uzinduzi hata kabla ya kumalizika kwa mwezi wa Ramadhan, tumeona ni busara kutoa fursa kwa mashabiki wetu ambao ni Waislam ili kujiandaa na swaumu," alisema malkia au '#Mama #mukubwa'.

"Tarehe rasmi itatangazwa ili wapenzi na mashabiki wote washuhudie Uzinduzi huu wa aina yake ambao naamini haujawahi tokea katika ulimwengu huu wa mipasho". Aliongeza Malkia wa Mipasho.

Huyo ndo Malkia mwenyewe kasema, sisi yetu macho na Masikio...!!!


Baadhi ya Wasanii Nyota wa Ogopa Kopa's