TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, August 25, 2015

Download Nyimbo Mpya ya Professor - "I love u mara millioni". Kuna watu wanaimba bwana...!!!!


Anaitwa Professor MK katoa kibao chake murua cha Taarab.
Katika kuonesha umahiri wake, nyimbo inaitwa "I love u mara millioni" ni msanii kutoka Wajela jela Zanzibar.

Download na kusikiliza hii nyimbo safi kabisa, kuna watu kumbe wapo wanaimba...!!!

TAMASHA LA COST NITE KUAHIRISHWA...!!!


Mratibu wa tamasha la Coast Nite Bw Emmauel ameeleza sababu zilizo pelekea kuailishwa kwa tamasha hilo lililo kua lifanyike ijumaa tar 28/8 escape One. 


Mratibu huyo kwanza amesema gharama ya kibali cha kufanya tamasha iko juu sana.
Pili kibali cha kuingiza wasanii toka nje ya nchi pia kiko juu sana na
Tatu kodi wanayo takiwa kulipa wasanii toka nje ya nchi ni kubwa ambayo them mashurooms wameilalamikia.

Mwisho Bw Emmanuel ametumia nafasi hii kuyashukuru makampuni yaliyo jitokeza kudhamini tamasha hilo ya precision air, clouds, push, ic, dasami, kapari, eventlites na mwananchi na kuahidi udhamini huo utatumika hapo mbeleni.

Kiongozi wa Them Mashurooms Band Bw John Katana amesema hawakuwa tayari kulipa kodi ya asilimia 15 kutoka kwenye mapato yao kwa kuwa kwanza iko juu sana ukilinganisha na kwao pili awakupewa taarifa mapema juu ya kodi hiyo hivyo anatalajia waandaaji kampuni ya On Point Solutions Ltd watazingatia hayo watakapokuwa tayali hapo baadae.

Friday, August 7, 2015

Download AUDIO MPYA: Mr & Mrs Hammer Q - Vijumba Jumba - Wamekuja ki - Vingine...

Mr & Mrs Hammer Q
Ni Mr & Mrs Hammer Q katika nyimbo Mpya waliyoipa jina la "Vijumba Jumba".

Ni nyimbo Tamu, Nyimbo nzuri iliyo tofauti kabisa na Miondoko ya Taarabu za hivi sasa, ni Taarabu asilia iliyoimbwa na watu wawili Mr & Mrs, wakiimba kwa kupokezana, utaipenda.

Hammer Q ameongea na blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com na kusema yupo katika mkakati kabambe wa kurudisha Taarabu asilia ile Taarabu ya kipindi kileee...!!

Ni nyimbo nzuri kusikiliza na Familia yako, Sherehe na Popote pale unaisikiliza kwa raha zako.


Download hapa uisikilize:-

Saturday, August 1, 2015

ANGALIZO: Viwanja vya wasanii wilayani Mkuranga...

Mkurugenzi wa Global One Group Bw Adam Emmanuel amewataka wasanii kua makini katika swala zima la umiliki wa ardhi.

Bw Adam ametoa angalizo hilo kufatia kupewa taarifa ya uwepo wa viwanja kwa ajili ya wasanii wilayani mkuranga mkoa wa pwani jambo lililo mfanya kufika ofisi ya aridhi wilayani humo na kupewa taratibu za kupata kiwanja katika maeneo yaliopimwa kwanza unanunua fomu tsh 15,000 pili ombi lako likipita kwa kiwanja cha makazi sq mita 1 ni tsh 3,250/ na ujazo wa chini ni sq 400 na baada ya hapo unasubili hati inapokua tayari unalipia tsh 20,000/ na kukabiziwa hati yako.

Hivyo swala la viwanja vya wasanii kwa garama ya tsh 50,000/ linaleta mashaka makubwa sana utalatibu wa kupata kiwanja halali cha serikali unalipia 15,000/ ya fomu ya maombi, ukipata unapewa ofa na unatakiwa kulipia tsh 3,250/ kwa sq mita 1 na unapoitwa kuchukua hati unalipia tsh 20,000/ unakabiziwa hati yako, malipo yote yanafanyika kupitia benk ya NMB.

Hofu hii inakuja kwa kuwepo taarifa ya viwanja vya wasanii kwa garama ya tsh 50,000/.


Onyesho la COAST NITE lasogezwa mbele kidogo...


Onyesho la COAST NITE na THEM MASHUROOMS BAND toka kenya lililo kua lifanyike leo Jumamosi tar 1/8/2015 sasa kufanyika Ijumaa ya mwisho wa mwezi huu pale pale ESCAPE ONE mikocheni.

Karibuni sana na Poleni kwa usumbufu / Mabadiriko haya.

UNAWEZI KUAMINI KUWA TANZANIA HAKUNA TAARAB SIKU HIZI...!? Muziki wa Taarab unautata ...! HEBU SOMA HAPA...

-->
Muziki wa Taarab unautata wa vyanzo viwili.

1. Kuna wanaosema taarab iliingia nchini mwetu kupitia ikitokea Mombasa.

2. Kuna tafiti nyingine ambazo zinaonyesha Sultan Barghash wa Zanzibar aliwapeleka wanamuzikiwawili Misri kujifunza upigaji wa Taarab,na hao waliporudi ndo walipanda mbegu ya Taarab nchini mwetu.

Taarab imekuwa nahistoria ambayo ya kuwa na aina nyingi za taarab, na mpaka leo mabadiliko ya taarab yanaendelea. Imefikia sasa kuna hata vikundi vya taarab vina wacheza show. Taarab imekuwa pia ni ya kucheza na si kusikiliza ujumbe tu kama ilivyokuwa zamani.

-->


Tunaweza kukubaliana mabadiliko katika kila kitu kwamba hata binadamu ana mabadiliko ya marika yaani utoto, ujana, umakamo, uzee hatimaye ukongwe.

Mabadiliko haya ya kimaumbile hayamfanyi mtu/binadam abadilike kuwa ngedere. Lakini si vyema kumfananisha au kughafilisha wasifu wa mtu/mwanadamu na ngedere. Kwa sababu mtu/mwanadamu asilani atabaki kuwa mtu/mwanadamu hali kadhalika ngedere asilani atabaki kuwa ngedere.

Taarab ni taarab na huu muziki mpya ambao bado haujapata jina kamili iwe ni mipasho au rusha roho utabakia kuwa rusha roho au mipasho na asilani huwezi kuwa taarab.

Kuhusu maswali ya hapo juu yanaweza kujibiwa na tafiti nyingi kuhusu muziki wa Taarab zilizoandikwa na kurekodiwa na taasisi na watafiti mahiri wa muziki (Outstanding Musicologists) kama vile kina Said A.M. Khamis, Werner Graebner, Mohamed El-Mohammady Rizk, K.M. Askew, Global Music Centre na vyuo vikuu mbali mbali hususani vya Ulaya na Marekani.

ZAIDI: Said A.M. Khamis anapagawishwa na mabadiliko katika nidhamu ya muziki wa Taarab - Wondering About Change: The Taarab Lyric and Global Openness. Nordic journal of African Studies 11(2): 198-205 (2002). Said A.M. Khamis* University of Bayreuth, Germany. (http://www.njas.helsinki.fi/pdf-files/vol11num2/khamis2.pdf). Nadhani Bwana Said A.M. Khamis tupo kwenye upande mmoja wa mtazamo kwamba hii iliyokuja sasa ni mipasho au rusha roho ni aina nyingine ya muziki na siyo taarab.





-->
Wengi wanapagawishwa na mabadiliko yanayoendelea ambayo yanatokana na sababu nyingi, lakini pia ni vizuri kujiuliza kama taarab "halisi" ni ipi ambayo ndicho kipimo cha taarab.

Kipimo changu cha taarab halisi kinaanzia kwenye tungo (Ushairi wenye vina na maudhui au hata kama ni bashrafu ni bashrafu iliyopigika katika mtindo na ala za okestra ya taarab).

Tofauti nyingine imelalia kwenye muziki wa Taarabu: kimuziki (ala zitumikazo, mtindo wa muziki unaopigwa kimapigo (Rhythm), ghani (melody), na mwafaka (harmony). Halafu linakuja suala la nidhamu ya muziki wa taarab: Mtindo wa utumbuizaji wa muziki wa taarab (presentation style) kuanzia wajihi wa wanamuziki (performers personalities), muundo ukaaji jukwaani (stage arrangement), mtindo wa jukwaani na majukwaa (stage setting and arrangement), mazingira ya utumbuizaji (performance aura), wahudhuriaji na aina wahudhuriaji onyesho (audience and audience target/ audience demography). vigezo hivyo nilivyovitaja na vinginevyo ndivyo vinavyoitofautisha taarab na chakacha au na mipasho au rusha roho.

Kabla ya mipasho na rusha roho palikuwepo chakacha lakini haikuwahi kutokea kuchanganya taarab na chakacha. Au siyo?

Haya mambo ndiyo ya kutaka serikali ya sultani iteue Sultani mwanamke. Ikishateuliwa Sultani mwanamke huo si usultani tena. Au Vatikani wamchagua Papa mwanamke, ikitokea kuchaguliwa papa mwanamke huo si Ukatoliki tena.

Vivyo hivyo ikiwa kama taarabu itapigwa kwa ala za muziki wa dansi, na wacheza shoo tena shoo hizi za kiwana mipasho, na tungo zisizo za kishairi na maneno yasiyo na staha, na kupigwa kwenye kumbi za vilevi basi hiyo si taarab ni mipasho au rushaa roho na si taarab.

Hebu niambie leo ukute watu wanapiga muziki wao kwa kutumia accordian, gitaa baridi na manyanga halafu wakuambie hii ni heavy metal, utaafikiana nao au utafikiri wamepatwa na ugonjwa wazimu.