TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, June 6, 2015

UZINDUZI WA #OGOPA KOPA'Z WASOGEZWA MBELE"...

Malkia Khadija omary kopa
ULE uzinduzi wa kundi jipya la mipasho Tanzania, #Ogopa kopa'z uliyokuwa ufanyike Juni 13 mwaka huu 2015, ndani ya #Escape One, jijini Dar es salaam, umesogezwa mbele ili kuupisha mwezi mtukufu wa #Ramadhan.

Mkurugenzi wa kundi hilo, Malkia Khadija omary kopa alisema jijini Dar es salaam jana akiueleza mtandao huu wa taarabuzetu.blogspot.com kuwa, Uongozi wa juu ndani ya kundi lake ulifikiria makubaliano ya kuusogeza mbele uzinduzi huo:-
"Tunaomba radhi mashabiki wetu na tunaahidi kutangaza tarehe nyingine ya uzinduzi hata kabla ya kumalizika kwa mwezi wa Ramadhan, tumeona ni busara kutoa fursa kwa mashabiki wetu ambao ni Waislam ili kujiandaa na swaumu," alisema malkia au '#Mama #mukubwa'.

"Tarehe rasmi itatangazwa ili wapenzi na mashabiki wote washuhudie Uzinduzi huu wa aina yake ambao naamini haujawahi tokea katika ulimwengu huu wa mipasho". Aliongeza Malkia wa Mipasho.

Huyo ndo Malkia mwenyewe kasema, sisi yetu macho na Masikio...!!!


Baadhi ya Wasanii Nyota wa Ogopa Kopa's

0 comments:

Post a Comment