TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, June 27, 2015

Bendi ya Them Mushrooms kutua Dar es Salaam!!!!

Wasanii wa Them Mushrooms
Kuna tetesi zinazodai kuwa bendi ya Them Mushrooms ya jijini Nairobi inatalajiwa kutua jijini Dar kushiliki kwenye tamasha la COAST NITE linalotalajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza hapa Tanzania mwezi wa nane.

Tamasha hilo ufanyika mara mbili kila mwaka jijini Nairobi kwa kuzishilikisha bendi za taarab toka hapa nchini Tanzani.

Bendi zilizo wahi kushiriki kwenye tamasha hilo ni New Zanzibar star, The East African Melody, TOT taarab, Mashauzi na Dar Modern.
Kwa mwaka huu jijini Nairobi tamasha hilo litafanyika ijumaa ya tar 6 mwezi wa kumi (06/10/2015) na moja na bendi itakayo kwenda itajulikana mwezi ujao wa saba.


Coast Nite ni tamasha lililo sajiliwa Nairobi na sasa tunalisajili Tanzania hivyo litakua linafanyika Nairobi na Dar kila mwaka Lengo letu ni ifikapo 2017 iwepo Afika Mashariki nzima Kenya, Tanzania, Rwanda, Burundi na Uganda kwani kote huko mazungumzo yanaendelea vizuri. Mmoja wa waandaaji wa Tamasha hilo aliimegea Blog hii ya Taarabuzetu.blogspot.com 

0 comments:

Post a Comment