TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, March 21, 2014

MPAMBANO: Hadija Yusuph amgalagaza Isha Mashauzi...

Jana Alhamisi ya Tarehe 20 Machi kulikuwa na mpambano mkali wa nani muimbaji mzuri wa Taarab kati ya Hadija Yusuph wa Jahazi na Isha Mashauzi wa Mashauzi Classic.

Mpambano huo ulifanyika katika kipindi cha Ambaa na Mwambao ndani ya Passion FM kikiongozwa na mtangazaji machachari Warda Chande aka "Mwana Dar es Salaam".

Mpambano huo umetokana na mabishano makali baina ya wapenzi wengi wa Taarabu na kupelekea kuandaliwa kwa mpambano huo.

Mpaka mpambano unamalizika ukiwa na wapiga kula kumi na sita (16) katika simu na Msg, Kura 12 zikisema Hadija ni bora zaidi na 4 zikisema Isha ni bora zaidi.

Mpambano huu nauleta kwako mdau utoe maoni yako ni nani zaidi!?
Hadija au Isha!?

3 comments:

Anonymous said...

Khadija Yussuf

Anonymous said...

Isha mashauzi zaidi

Anonymous said...

Isha mashauzi yuko juu

Post a Comment