TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, July 24, 2014

Ujio wa Black Kopa mtoto wa Khadija Kopa, ni Sheedah...!!!!

Anakwenda kwa jina la Muhammed Kibwana au Black Kopa pia unaweza kumuita Prince Kopa, mtoto wa Malkia wa mipasha Tanzania Bi Khadija Kopa.

Ni msanii wa Muziki toka muda mrefu kama ilivyo kwa Mama yake, marehemu kaka yake (Omary Kopa) "Apumzike kwa amani", pamoja na ndugu zake wengine wamekuwa na kipaji cha kuimba karibu familia nzima.

Black Kopa yeye anasema ameanza kuimba siku nyingi akiwa amejikita sana katika mziki wa Bongo flaver na ameweza kutoa nyimbo kadhaa, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda, marafiki na familia yake pia wakawa wanamshauri ni kwanini asiimbe taarab wakati sauti nzuri ya kuimba anayo!?.

Hatimae kijana kaamua kujitoa mazima mwaka 2014 na kuachia nyimbo yake inayokwenda kwa jina la "Full kuenjoy".

Black Kopa akihojiwa na Blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com
Anasema nyimbo hii inapatikana katika albam ya Ogopa Kopa's Classic Band" ambayo ni bendi changa na ni mpya kabisa inakuja hivi karibuni. Albam itaitwa "Lady with Confidence".

Katika nyimbo hii ameshirikiana na watu takribani wanane, wanne wapiga vyombo na wanne waitikiaji.

Waitikiaji ni:- 1). Warda Mlawa, 2). Shadya Shombeshombe 3). Rukia Manala na 4). Hemed Omary.

Wapiga vyombo ni:- 1). Omary Zungu au Omary Kinanda (Keyboard) 2). Harifa (Keyboard 2), 3). Miraji (Soro Gitaa), 4). Said James au Said Bass (Bass Gitaa).

Black Kopa anakuja kwa kasi anasema mashabiki wajiandae kupata radha mpya kabisa toka kwake na atafanyia remix pia nyimbo za kaka yake Omary Kopa kwa kuziimba.

Mashabiki anaomba saana sapoti yenu.

0 comments:

Post a Comment