TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, July 4, 2014

UJUMBE MZITO WA HAMMER Q KWENDA KWA #LIL GETTO WA AKHENATON RECORD...

Hammer Q
 Nimepata data zako bob

Lakini Na amini kuwa MUNGU pekee ndie ana mamlaka ya kuamua lolote juu yangu na sio wewe Nitakupenda km binaadam mwenzangu hata km nimestuka kuna mabaya unayonitendea naamini hujui ulitendalo...!

Nitaendelea kuishi kwa uhalisia wa maisha yangu na ilivyoumbwa roho yangu sitakulipiza baya lako kwa baya langu sababu Mimi kwa sasa nimekua sio mtu wa visasi na roho yangu ni nyeupe kabisa sitakutendea baya bali nitakuombea kwa mungu akubadilishe kutoka roho mbaya uliyonayo na akuongoze ktk njia sahihi

Jifundishe kuTii haja za moyo wako si maneno ya watu...! Kawaida Yangu huridhika na nilichonacho kwa kuamini ndicho MUNGU alichonipa na kuna siku nitapata zaidi...! Na unavyonidharau nitazid kukuheshim na kujituma maana unanipa uchungu wa kutafuta mafanikio...!

Huwa na Amini na mimi ni muhimu ktk jamii ndio mana nimeumbwa...! nakushangaa sana unavokua mtu wa kujaribu kuniharibia rizki zangu kana kwamba umeziumba ww Nasijui ingekuaje kama ungepewa funguo ya rizki

We Fanya unavofanya niharibie unavoniharibia mimi namuachia Mungu kisha Nikutakie ramadhan NJEMA Na mungu akutilie wepes ktk kubadilika .ningekusema pembeni ningemkosea mungu lkn nimekuchana kweupe kuridhisha roho yang.

Bob (Lil Ghetto).
Blog hii ilimpigia simu Hammer Q ili kujua ni nini kilichopelekea yeye kuandika ujumbe mzito namna hii kwenda kwa Bob (Lil Ghetto)

"Unajua huyu jamaa ni mbinafsi sana, mimi baada ya kujiunga nae sikujua kitu lakini nimekuja kuona mambo yake sio kabisa ndo nikaona bora nijitoe tu nifanye mambo yangu mimi kama mimi, lakini hata baada ya kutoka amekuwa akinifuatilia sana, hapa juzi tu tena kanifanyia fitna katika jitahada zangu za kujitafutia ndo nikaamua kuandika ujumbe huu na ninaamini utakuwa umemfikia. Sijaandika kwa siri nimeandika kweupe nikiwa na uhakika wa ujumbe kumfikia mlengwa!". 


Katika kundi la Offsidetrike liliokuwa likiongozwa naye Lil Ghetto na Hammer Q kwasasa yupo Lil Ghetto mwenyewe (Pekee).

0 comments:

Post a Comment