TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, January 24, 2014

AMIN SALMIN:- T Moto haijafa na wala haitakufa...

Mkurugenzi wa Bendi ya T Moto Amin Salmin amefunguka kwa kusema kuwa, T Moto ipo ngangari haijafa wala haitakufa na hivi karibuni itaanza harakati zake kwa nguvu mpya.

Amin alisema hayo baada ya tetesi kutoka kwa wadau mbalimbali wa taarabu kuulizia katika blog hii siku chache zilizopita.

Amin Salmin alisema:- Mimi ndio mmiliki wa T Moto, kweli bendi imekua kimya kwa muda sasa hii kutokana na sababu kuu mbili:- Moja T Moto nilivunja uongozi wa kuisimamia bendi ukinitoa mm wakati nafanya hayo kwa bahati mbaya nami nikapata ajali na bendi kubaki chini ya wasaanii wenyewe nao baada ya muda wakashindwa kuiendesha ndipo nikazuwia maoshesho kwa muda ili kujipa muda wa kijiuguza kwa muda wa miezi sita, nilikua mgonjwa ila kwa ss nashukuru nimerudi ktk hali yangu ya kawaida, "T Moto haijafa na wala haitakufa" karibuni tu itaanza harakati zake na kutoa upinzani km kawaida tunawaomba mashabiki na wapenzi wategemee uhondo kutoka kwetu kwani tunajua nini wanapenda na nn tuwafanyie.

Wale wapenzi wote wa burudani na wadau wa T Moto habari ndo hiyo, Bendi ipo karibu kuingia kambini.


Picha zikionesha Mkurugenzi wa T Moto Mr. Amin akiuguza mguu wake.

Amin hapa akiwa na hali nzuri kiasi karibu kuingia mzigoni.




0 comments:

Post a Comment