TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, January 22, 2014

NDAGE NDAGE SI MSANII WA SUPERSHINE TENA - "KAIS MUSA"

Ndage Ndage.
Kais Mussa Kais Manager wa Supershine.
Msanii na mpiga kinanda maarufu Ndage Ndage ameondoka katika bendi ya Supershine bila kuuaga uongozi.

Taarifa za kutoweka kwake zimezungumzwa na Meneja wa Supershine Modern Taarab Mr. Kais Musa kwa kuiambia blog hii kuwa:-
Ndage Ndage alikuwa msanii wetu, tumempangishia Chumba kwa miezi sita lakini ameka kwa kipindi kidogo tu akadai salio kwa mwenye Nyumba akarudishiwa, akauza vitu tulivyomnunulia kama Godor na Feni (Pangaboy) kisha akatoweka. Kais alisema.



Aliongeza kwa kusema, kutokana na kuonesha utovu wa nidhamu wa hali yajuu hatumtaki tena na hatuhitaji kuwa naye kwenye bendi maana tunawapiga kinanda wakutosha na Bendi iko poa imesimama vya kutosha.

Katika pekua pekua na juhudi ya mwandishi wa blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com ili kupata habari zaidi, ilimpigia simu Ndage na simu yake ikawa haipatikani kwa muda mrefu, baada ya kuwa hapatikani, zikapatikana taarifa kuwa: Ndage aliuza vitu pamoja na kurudisha Chumba ili apewe salio lililopo kutokana na kuugua hivyo kutokuwa na pesa ya kujitibia na yeye mwenyewe kurudi nyumbani kwao.

Taarabuzetu tunawasihi wasanii wote wa Taarabu kuwa na nidhamu kwa viongozi kuwashirikisha matatizo yenu ili kujua ni kitu gani kinaweza kufanyika, mtu wa kuendeleza muziki huu wa Taarab ni wasanii wenyewe.

2 comments:

Anonymous said...

huyo ndio ndage ndage bana teja liliokubuhu

Anonymous said...

Wasanii wanashindwa kutumia nafasi wanazopewa... Ni shidaaa...!!!

Post a Comment