TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, January 31, 2014

DAR MODERN TAARABU YATAMBULISHA WASANII WAPYA NA ALBUM MBILI...

Baadhi ya wasanii wa Dar Modern Taarabu.
Kundi maarufu la miondoko ya Taarabu nchini Dar Modern Taarabu jana Alhamisi limetambulisha wasanii wapya watakaoungana na wasanii wengine kuunda kundi na kuboresha zaidi.

Akizungumza na blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com katika kikao walichokiandaa makamu wa Rais wa Bendi hiyo Bakari Hassani amesema wamechukua wasanii wengi kutoka bendi tofauti tofauti ili kuboresha bendi na kukabiriana na ushindani uliopo.
Baadhi ya Viongozi wa Dar Modern katika Mkutano wa jana wakiwa na baadhi ya wasanii.
Makamu huyo wa Rais aliwataja wasanii waliowachukua ni:-
- WAIMBAJI WAPYA NI HASSAN VOCHA ALIYEKUWA KWA SAID FELLA (G5 MODERN)
- ZUBEDA MLAMALI KUTOKA NEW ZNZ STAR,
- MWAMVITA SHAIBU, MOSSY SULEIMAN NA BI MWANAHAWA ALLY WOTE WAMETOKEA 5 STAR MODERN TAARAB,
- AMOUR MAGULU,
- RAMADHAN KISOLO KATOKEA MASHAUZI NA 

- MGENI KISODA WA JAHAZI (5STARS)

Pia katika mkutano huo uliokuwa umehudhuliwa na waandishi mbalimbali wa habari nchini, Dar Modern waliweza kutambulisha Album zao mbili kwa pamoja ambazo watazizindua tarehe 14 Feb siku ya wapendanao katika ukumbi wa Travertine Magomeni.

Album alizitaja kuwa ni:
1. KITWITWI - IMEIMBWA NA SIKUDHANI ALLY NA 
2. OH! MY HONEY IMEIMBWA NA HASSAN VOCHA.

Katika album hizo kutakuwa na nyimbo kama:-
1. Kitwitwi

2. Oh my honey
3. Sikuamini macho yangu
4. Siwanyimi uzuri

NYINGINE NI:-
1. Malipo Duniani
2. Naenda kwa Mume wangu
3. Ngoma imepasuka

Nyimbo zote zimetoka na baadhi zimeshaanza kusikika radioni, Mr. Bakari amesema pia baadhi ya nyimbo zingine zipo katika maandalizi zitaingizwa katika album hizo.

WADAU WOTE WANAKARIBISHWA SIKU YA VARENTINE 14 FEB PALE TRAVERTINE MAGOMENI KUJA KUPATA BURUDANI YENYE RADHA MPYA KUTOKA DAR MODERN TAARABU MPYA YA 2014.

1 comments:

Anonymous said...

jaman tunataka ukweli kuhusu dida n temba mbona ham2pi udaku ha ha ha

Post a Comment