TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, January 16, 2014

OFFSIDE TRICK WAACHIA NGOMA MPYA:- TALAKA ...

Kundi machachari la miondoko ya miduara Tanzania Offside Trick linaloongozwa na wakali wawili Hammer Q na Lil Gheto Jana January 15, 2014 limetambulisha single yake mpya inayokwenda kwa jina la TALAKA.

Akizungumza na blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com msanii wa kundi hilo Hammer Q alisema single hii ni kati ya nyimbo zinazokamilisha album yao mpya itakayotoka hivi karibuni, "nyimbo zote za album nzima zimekamilika na hii ndio ilikuwa nyimbo ya mwisho".

Alipoulizwa ni kwa nini single hii wameipa TALAKA!? Hammer Q alisema, siku hizi Talaka imekuwa ni kitu cha kuwaida tu kutokana na kudanganyana katika Mapenzi, watu wanafunga ndoa leo week moja wanaachana "Ni kama umeenda kununua Vocha" yaani hawaoni taabu, mtu anatoa Talaka kama anagawa Vipeperushi...!!

Wapenzi wa Mduara kaeni tiyari kuipokea Album ambayo itakuwa na ladha kibao za mduara halisi toka kundi bora kabisa la Mduara Tanzani Offside Trick "Watoto wa Kizanzibari".

SIKILIZA NA DOWNLOAD HAPA "TALAKA".


0 comments:

Post a Comment