TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, January 10, 2014

FATMA ALLY (MAMA SHUGHULI) AWAPASHA WATANGAZAJI WA VIPINDI VYA TAARABU.

Fatma Ally (Mama Shughuli) kushoto akiwa na Warda Chande wa Passion FM.
Anaitwa Fatma Ally au ukipenda muite Mama Shughuli, ni muimbaji wakutumainiwa katika bendi ya Jahazi Modern Taarabu.

Jana akizungumza na Warda Chande wa Passion FM katika kipindi cha Ambaa na Mwambao kinachosikika mida ya saa Saba mpka saa Kumi za jioni aliongelea mambo mengi sana yahusuyo muziki na maisha yake kidoogo.


Katika maongezi yake Fatma aliongea kuhusu kukerwa kwake na baadhi ya watangazaji wa vipindi vya Taarabu kwa tabia yao ya kuacha kuzungumzia nyimbo pamoja na waimbaji wake na badala yake wanatumia nyimbo hizo kutengenezeana vijembe kwa watu walio na chuki nao halafu nyimbo inakuja kuonekana na ujumbe tofauti.

"Watangazaji wa vipindi vya Taarabu wamekuwa wakitumia muda mwingi kujisifia, kujisema wao na kuwazungumzia watu wengine kwa kuwapa vijembe vya taarabu katika nyimbo tunazoimba badala ya kuzichambua na kuzizungumzia, tabia hiyo kwakweli huwa siipendi naomba wabadirike!" Alisema Fatma.

Fatma ni msanii wa siku nyingi na amejaribu kulinganisha muziki ule wa zamani na wa sasa akasema muziki wa sasa umekosa maadili, umezidi Matusi na Vijembe vya waziwazi kati ya wasanii kwa wasanii, unatunga nyimbo na kuiimba lakini anatokea mtu mwingine anakujibu kwa kukukejeli... Mambo kama hayo hayakuwepo zamani.

Fatma Ally a.k.a. Mama Shughuli kabla ya kujiunga na Jahazi alikuwa katika Bendi ya Babloom.
Akiwa Jahazi ameweza kuimba Nyimbo kama:-
Ng'ombe wa Maskini,

Shukurani ya Punda na
Hata bado hujanuna.

2 comments:

Anonymous said...

yap

Anonymous said...

safi xn kwa kuwachana nimeependa xnaaa wanatuchefuwa tuuu

Post a Comment