TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, January 29, 2014

WAKALIWAO MODERN TAARADANCE YAKAMILISHA TATU KALI...! SALHA WA HAMMER NDANI...!!!

Mkurugenzi wa Wakaliwao Thabit Abdul "Jiko la Jela".
Wakaliwao Modern Taaradance ni kundi la Taarabu lililoanzishwa hivi karibuni na mkongwe wa muziki hapa nchini anayejulikana kwa jina la Thabit Abdul a.k.a Jiko la Jela.

Kundi hili baada ya harakati za hapa na pale hivi sasa limefanikiwa kuipua nyimbo zake mpya tatu (3) chini ya Producer/Director Thabit Abdul

Mkurugenzi huyo (Thabit) alizungumza na Blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com na kuzitaja nyimbo hizo ambazo ni za kuanzia tu katika ujio wa Albam, alizitaja ni:-
1. Kalieni Viti sio Umbe - Imeimbwa na Hamuyawezi Kondo
2. Subira haina Kikomo - Imeimbwa na Asia Mariam
3. Sema na Mume wako - Imeimbwa na Farida Kindamba

Pia katika kukamilisha Albam nzima itakayokuwa na jumla ya nyimbo Sita (6).
Nyimbo zitakazokamilisha Albam alizitaja kuwa ni:-
4. Naishi Naisha - Ataimba Mwalim
5. Watu na Bahati zao - Ataimba Aisha
6. You and Me - Ataimba Thabit

Warda Chande "Mwana Dar esSalaam" Mtangazaji wa Passion FM katika Kipindi cha Taarabu - Ambaa na Mwambao akipozz na Thabit Abdul baada ya Mahojiani.

Akihojiwa na mtangazaji Warda Chande wa Passion FM katika kipindi cha Ambaa na Mwambao Thabit alisema Nyimbo zote hizo ni Utunzi wake, Kinanda, Solo na Vingine vyote Sijui Director vyote kafanya mwenyewe... Ni Hatareeee...!!!!

Amesema Albam itakuwa tiyari kabla ya Sikukuu ya Pasaka ambapo ndo itakuwa uzinduzi rasmi ila kwasasa wanafanya show zao siku mbili kwa wiki:-
** Kila Jumatano CHITOZ Kijitonyama (Miti mirefu) na
** Kila Ijumaa Y Bar - Kinondoni Moscow (Nyumbani)

Mkurugenzi huyo wa Wakaliwao alisema bendi yake amesheheni vichwa vikali na vyenye vipaji na amechukua wasanii wasio na majina maalufu isipokuwa wawili tu ambao ni wakongwe katika gemu:-
* Abdul Misambano ambaye atakuwa kama mlezi wa Bendi
* Salha wa Hammer - ambaye atatikisa bendi zote za taarabu kwa umahili wake katika kuimba.

Pia wanahitajika wataalamu wa kupiga Solo na Base! Thabit amesema ni lazima wawe wakali kama au kumzidi yeye katika kucharaza vyombo hivyo. (Nafasi ya kazi hiyo).

Thabit Abdul amewaomba wadau wa mziki wa Taarabu hapa nchini na nchi za nje kumsapoti na kujiandaa vyema katika uzinduzi wake siku hiyo ya Passaka

0 comments:

Post a Comment