TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, November 11, 2013

DEALER'S MODERN TAARABU, WAIBIWA VIFAA VYA MUZIKI...

Bendi mpya ya Dealer's Modern Taarabu inayoongozwa na Mwanahawa Ally Chipolopolo imeibiwa vifaa vya muziki. 

Bendi hiyo iliibiwa vifaa vyake vya muziki vikiwa stoo baada ya kumaliza show yake, vifaa vilivyoibiwa vimetajwa zikiwemo Mic 5, Wire za Mic 5, wire za Vinanda 2 pamoja na vifaa vingine ambavyo thamani yake ni zaidi ya laki nane. 

Akizungumza na mwandishi wa blog hii ya Taarabu Zetu Mkurugenzi wa bendi hiyo Mwanahawa Ally "Chipolopolo" alisema wizi huo ulitokea Tar 3 wakati yeye yupo Travetine katika show ya DIDA wa times.

Mpaka sasa mwizi hajapatikana ila mlinzi aliyekuwa zamu siku hiyo ndo anashikiliwa.

1 comments:

Anonymous said...

Huyo mlinz aeleze kinagaubaga hivyo vifaa vimekwenda wapi

Post a Comment