TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, November 1, 2013

MAZOEZI YA BENDI MPYA ROCKY CITY MODERN TAARABU YASUASUA.

Bendi mpya iliyoanzishwa wiki moja iliyopita ya ROCKY CITY MODERN TAARAB imeanza kupata ugumu wa tasnia hii kutokana na miundombinu mibovu waliyonayo haswa kifedha kuwayumbisha. 

Akizungumza na Mwandishi wa blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com kwa sharti la kutotajwa jina lake mpiga gitaa wa bendi hiyo alisema kwamba wanafikiria kusimamisha mazoezi ya kuandaa nyimbo mpya mpaka pale watakapojipanga upya kuhusu fedha, kwani mpaka sasa uongozi huwa una nunua chakula kwa baadhi ya wasanii na jioni unatoa elfu 3 kama nauli kwa baadhi ya wasanii jambo linalofanya wengine kulalamika.

0 comments:

Post a Comment