TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, November 1, 2013

WASANII G5 MODERN TAARABU, WAANZA KULALAMIKIA UONGOZI..

Bendi ya G5 Modern Taarabu imeanza kukumbwa na mtikisiko baada ya baadhi ya wasanii kufikisha malalamiko yao katika ofisi zetu kwamba wamekuwa wakipigwa danadana kila kukicha na uongozi wao haswa mkurugenzi wao. 
"Unajua wakati tunaanza hapa G5 kila msanii alikuwa na matumaini kwamba mambo yatakuwa mazuri kimaslahi kutoka na maongezi ya ahadi nono, lakini kadri siku zinavyosonga mambo yamekuwa yakibadilika tu, hakuna tunachokielewa. sisi wengine tuna familia, tuna watoto ambao hawana baba, sasa unaponidanganya unakuwa hunitendei haki". alisema msanii mmoja ambae alikataa kutajwa jina lake!.

0 comments:

Post a Comment