TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, November 8, 2013

HATIMAE BI MWANAHAWA ALLY NA BI AFUA SULEIMAN WAPATANISHWA...!!

Bi Afua Suleiman na Bi Mwanahawa Ally.
Wakongwe wa taarabu nchini Tanzania Bi Afua Suleiman na Bi Mwanahawa Ally ambao walikuwa na uhasama mkubwa, wamepatanishwa na kwa sasa sio mahasimu tena!. 

Akizungumza na mwandishi wa blog hii Bi Mwanahawa alisema watu ndio waliokuwa wanatugombanisha, lakini kwa sasa tumewabaini na haitotokea tena kufarakana. 

Kwa upande wa Bi Afua yeye nae alimshukuru Mungu kwa kupatana na mwenzake na kuahidi kutosikia maneno yoyote kwani waja wamezoea kuyazua maneno. 

Ugomvi wa Bi Afua na Bi Mwanahawa ulikuwa ukiwagawa wapenzi..lakini kwa sasa yamekwisha.

0 comments:

Post a Comment