TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, February 6, 2014

AISHA VUVUZELA NA DUME MARIOO...

Aysher na AT wakiwa Studio wakianda "Dume Marioo".
Anaitwa Aysher Othman (Vuvuzela) msanii mwimbaji machachali wa Taarabu hapa Tanzania amegeukia kwenye Miduara.

Akizungumza na blog hii ya Taarabuzetu.blogspot.com Vuvuzela alisema tiyari ameshaingia Studio kurecord nyimbo yake ya mduara inayokwenda kwa jina la "DUME MARIOO" akiwa ameshirikiana na A.T.

Aysher pia amesema katika upande wa mduara Meneja wake ni AT na nyimbo hiyo imerekodiwa katika studio za AT pia.

Kuhusu Taarabu Aysher anasema yupo kama kawaida ila anachotaka kufanya ni kuwaonesha watu kuwa fani anaiweza kotekote maana anavipaji vingi na akiamua kuimba Dance anaweza pia.

Aysher yupo kundi gani kwasasa!?
"Nimerudi kings kwa majaliwa @ kabla Five Stars haijavunjwa rasmi@ na nyimbo itatoka mwezi wa 3 si sasa ila mkao wa kula kaeni hii ni sauti ya mtoto wa Uswahilini mwenye kipaji cha kuzaliwa si kuiga wala kubabaisha, ni sauti ya Vuvuzela".
Aysher Othman (Vuvuzela).
Wapenzi wote wa mduara na wapenzi wa Aysher Othman (Vuvuzela) wakae mkao wa kula kuweza kupokea radha mpya toka kwake

1 comments:

Anonymous said...

Lete mambo tuone kama unaweza Aysher...!!

Post a Comment