TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, February 14, 2014

AMIN SALMIN KUPIMA DAMU LEO 14 FEB SIKU YA WAPENDANAO....

Mkurugenzi wa T Motto, Mr. Amin Salmin.
Mkurugenzi wa bendi ya T MOTTO Amin Salmin leo Feb 14 atapima damu mbele ya waandishi wa habari. 

Amin Ameamua kuwa kinyume kidogo na walio wengi katika siku ya wapendanao. Siku hii yeye atakwenda AMREF mbele ya waandishi wa habari na atapima damu na atachangia kwa jamii kwaajili ya watu wasiojiweza na si vinginevyo. 

Akizungumza na mwandishi matata wa blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com Amin amesema jamii imekuwa ikipotoshwa na tamaduni za kimagharibi kwa kufuatisha mambo yasiyo wahusu wala kujua faida au hasara ya hicho wanachofuatisha. 

Siku hizi imekuwa ndio mtindo kwa jamii kujiandaa kwa ajiri ya ngono kwa kisingizio cha siku ya wapendanao!, huu ni upuuzi na ujinga upendo upo kila siku na sio tarehe 14 kama wanavyodanganywa!. 

 Ifike wakati tufanye mambo mazuri kwa ajiri ya taifa letu na sio kufuatisha mkumbo tu. 

Mtandao huu unatoa pongezi kwa mkurugenzi huyu wa T MOTTO kwa uamuzi wake wa busara ambao unapaswa kuigwa katika jamii yoyote ya wapenda maendeleo! 
Hongera sana AMIN SALMIN!.

0 comments:

Post a Comment