TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, February 26, 2014

SINA BAND, ANAYENIHITAJI NIKO TIYARI "ANIFA MAULID"...

Anifa Maulid "Jike la Chui".
Anaitwa Anifa Mohamed "Jike la Chui" mwimbaji machachari katika tasnia ya muziki wa Taarabu Tanzania, amefunguka kuhusiana na yeye yupo wapi kwa sasa.

Akizungumza na mwandishi wa taarabuzetu.blogspot.com Anifa amesema kwasasa hana bendi yoyote anayoifanyia kazi yaani yupo "Free" kwenda kuimba popote na yupo tayari kuingia mkataba na bendi yoyote itakayomuhitaji.

Amesema mala nyingi amekuwa akiimba katika jukwaa la TOT kama msanii mualikwa tu na si muimbaji wa TOT. Anakula "Ndondo".

Katika ujio wake mpya Anifa baada ya "Makavu Live" amekuja na nyimbo yake mpya inayokwenda kwa jina la "Naufunga Mtaa". Ni nyimbo ambayo ameimba kutokana na kisa cha ukweli mtaani kwao.

Nyimbo hii ametunga mwenyewe na kupata ushauri kidogo toka kwa Thabit Abdul, Kaptani Temba na Hemed Omary.

Nyimbo hiyo ameimba kwa kuitikiwa na wasanii wa Wakali wao Modern Taradance, Asia Bin Mariam na Muya walio chini ya Mkurugenzi Thabit Abdul Jiko la Jela.
Anifa kushoto akiwa na mtangazaji wa kipindi cha Taarabu "Ambaa na mwambao" Passion FM.
Anifa anamshukuru sana Khadija Kopa kwa kumpa ushirikiano mkubwa sana katika uandaaji mzima wa nyimbo yake kwani alikuwa naye kuanzia mazoezi mpaka kwenye kurekodi, ametoa ushauri mkubwa sana!!.

Ni nyimbo nzuri na ya ukweli, Isikilize utaipenda!.

0 comments:

Post a Comment