TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, February 28, 2014

Hashim Said:- Sitoshiriki tena tuzo za Kilimanjaro Music Awards...

Hashim Said "Mzee wa Majanga".
Sitoshiriki tena tuzo za Kilimanjaro Music Awards zimejaa ubabaifu kila mwaka nilishiriki mwaka jana nimegundua mapungufu kibao. Hayo ni maneno ya Msanii mwimbaji mwenye kipaji ndani ya Mashauzi Classic anayeitwa Hashim Said Igwee "Mzee wa Majanga" ameyasema haya akiongea na mwandishi wa blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com

Hashim alipoulizwa ni Mapungufu gani ameyaona!?

Mapungufu ni mengi sana hasa kwa washindi wa tuzo kujijua kuwa wanakwenda kuchukua hizo tuzo, yaani huwa wanapewa taarifa kabisa kuwa leo unapata tuzo! Sasa haya ni mashindano kweli au kupeana??? iko wapi nafasi ya watanzania wanaopiga kura?

Kiukweli Tanzania bado sana katika suala hili, tujifunze kupitia wenzetu mfano tuzo za KORA tuzo za KISIMA kule kenya mpaka tuzo za muziki kule Marekani, lakini sasa kwa mtindo huu wa kupeana kila siku badala ya kuwapa chachu wasanii hasa wanaochipukia watakuwa wanawapa chuki.

Nitakuja kushiriki iwapo baraza la Sanaa Tanzania likifanya marekebisho au kuanzisha Tuzo za Baraza na si hizi za watu binafsi zinazotoa tuzo kwa kujuana na kupeana. 
 
Mimi ni mwanamuziki wa siku nyingi hasa katika tasnia hii ya taarab, niliingia kwa mara ya kwanza mwaka jana nimejionea mwenyewe kiukweli sihitaji kushiriki tena nawaomba wasije wakaweka jina langu tena anavyonitunza mke wangu inatosha sanaaaa.

0 comments:

Post a Comment