TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, February 14, 2014

MASHAUZI KUFANYA BONGE LA SHOO MORO, DODOMA NA KILOSA...

Mashauzi Classic ikiongozwa na Super Woman Mkurugenzi mwenyewe Isha Mashauzi leo siku ya Valentine watadondosha bonge la show kwa wapendanao mji kasoro Bahari Morogoro.

Tarehe 14 Februali ni siku ya wapendanao, siku inayoadhimishwa Duniani kote.

Mmoja wa wasemaji wa Mashauzi alisema, siku hii ya Valentine watakuwa Morogoro katika maeneo ya Nanenane ndani ya BZhotel, Mashauzi wataimba nyimbo zao zote na wataimba pia nyimbo zao mpya zilizo katika Albam yao ya Tatu "Asiyekujua Hakuthamini", pia kutakuwa na Nyimbo za Albam ya Nne, ni full shangwe.

Baada ya Show ya nguvu Morogoro, kundi hili machachari la Mashauzi litaelekea Dodoma siku ya Jumamosi na kushusha show moja ndani ya Royal Village, show zitakuwa zilezile kali tu.

Katika ziara hiyo Mashauzi Classic siku ya Jumapili watakuwa ndani ya Kilosa katika ukumbi wa Babylon Hall.

Wakazi wa maeneo hayo mnaomba kuwa na maandalizi ya kutosha kuipokea mashauzi maana kutakuwa na burudani tu mwanzo mwisho, ndo kitu kinachowaleta huko.

0 comments:

Post a Comment