TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, February 6, 2014

TWAHA WA DAR MODERN TAARAB, AKANA KUMKIMBIA HASSAN VOCHA!....


Muimbaji wa bendi ya Dar-es-Salaam Modern Taarabu Twaha malovee amekanusha habari zilizoandikwa na baadhi ya mitandao kwamba amemkimbia Hassan vocha msanii mpya aliejiunga na bendi hiyo akitokea G5 Modern taarab!.

Akizungumza na blog hii makini Twaha alisema, mimi ni muimbaji ninae jiamini na najua kuimba ndio maana nimefanya kazi mpaka mapacha watatu katika dansi, kamwe siwezi kumkimbia Vocha!, kilichotokea ni kuwa mimi nilikuwa nasumbuliwa na maralia ndio maana hata katika mazoezi ya Dar Modern nilikuwa sionekani, pia sijajiunga na gusagusa, sikweli ni uzushi tu mtu anapokuona umehudhuria show ya bendi yoyote basi huzusha kuwa umejiunga nayo.

Nawaahidi na kuwahakikishia wapenzi wa Dar Modern Taarabu kuwa, nipo na nitaendelea kuwa nao, wasikose tamasha kubwa la Valentine tutakalolifanya pale Travertine Magomeni siku hiyo Wapendanao tarehe 14 February 2014, siku hiyo nitapanda jukwaani na kuimba.

0 comments:

Post a Comment