TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, February 17, 2014

MASHAUZI CLASSIC KUMIMINA UHONDO MANGO GARDEN MWISHO WA MWEZI HUU, MASHABIKI KUWA MAJAJI WA VIDEO YA ASIYEKUJUA HAKUTHAMINI

Mkurugenzi wa Mashauzi Classic Isha Mashauzi.

ALHAMISI ya tarehe 27 Feb, mwezi huu kutakuwa na tukio la aina yake katika ukumbi wa Mango Garden katika onyesho maalum la Mashauzi Classic. 

Mashabiki wa kundi hilo linaloongozwa na Isha Mashauzi, watapata fursa ya kuwa majaji wa video ya wimbo mkali “Asiyekujua Hakuthamini”. 

Ni kwamba siku hiyo video ya “Asiyekujua Hakuthamini” itatambulishwa rasmi huku mashabiki wakipewa nafasi ya kutoa kasoro kazi hiyo na kisha itakwenda kufanyiwa marekebisho ya mwisho (final editing). 

Meneja wa Mashauzi Classic, Suma Raga ameiambia Taarabu Zetu kazi hiyo imefanyika katika kiwango cha hali ya juu, lakini bado mwamuzi wa mwisho ni mshabiki wa Mashauzi Classic. “Kazi hizi tunazifanya kwaajili yao, bila wao sisi hatupo, kwahiyo tunaileta kazi mikononi mwao ili tupate maoni yao. Tutakuwa tukiendelea na mfumo huu hadi mwisho wa nyimbo zote za albam ya “Asiyekujua Hakuthamini” ambayo itabeba jumla ya nyimbo sita,” alifafanua Suma Raga.

Pia sku hiyo ya tarehe 27 Feb,
watatambulisha nyimbo tatu mpya zitakazokuwa katika albam ijayo ya nne ambayo itaitwa "Wasafi wa mavazi wachafu wa nafsi" mbili katika hizo ni utunzi wake Hashim Said (Mzee wa Majanga)

0 comments:

Post a Comment