TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, February 17, 2014

Aysher Othman a.k.a. Vuvuzela ametoa pongezi kwa wale wote waliofanikisha na kuhudhuria Harusi yake.

Aysher Vuvuzela au Mrs Saaleh Mkassy akiwa na mumewe mpendwa.
Ilikuwa ni mchana wa saa 7 Ijumaa 14 Feb, siku ya wapendanao Aysher Othman alifunga ndoa na bwana Saaleh Zakaria Mkassy baada ya mshuko wa swala ya ijumaa.

Usiku wa saa tatu siku ya jumamosi kulikuwa na party iliyofanyika katika ukumbi wa Kibo Garden Kimara Rombo.
Kings Morden Taarab ilisindikiza party hiyo kwa burudani nzuri kabisa na wadau wa ukweli walifurahia!.

Mamaa Zeka na Mamaa Dabo S nawashukuru sana...! ilikuwa raha kuolewa ni stara na wasaani wa Kings walinipa zawadi nawashukuru wote. Alisema Bi Harusi huyo.

"Ilikuwa ni siku ya furaha kwangu, kwa sasa naitwa Mrs Saaleh Mkassy mamaa Vuvuzela" Alisema Aysher.

"Natoa shukurani nyingi sana kwa wote waliofanikisha kufanyika kwa harusi yangu, wote waliohudhuria na waliochangia kwa namna moja ama nyingine nasema
ASANTENI SANA...!!!"

0 comments:

Post a Comment