TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, October 17, 2013

AMOUR SALEHE ZUNGU AITOSA G5 MODERN TAARABU.

Amour Salehe a.k.a. Zungu.
Yule mpiga kinanda alietangazwa kwa mbwembwe na majigambo mengi na bendi ya G5 kwamba wamemsainisha mkataba akitokea Oman amewaacha solemba na kutimka zake tena Oman kuendelea na maisha yake ya kimuziki. 

Taarabu zetu ilipata nyeti hizo: "Mimi nilijua tu zungu lazima awalize G5, yule si mkaaji hapa nchini" alisikika shabiki mmoja wa bendi hiyo katika Bonanza la kila jumapili ambalo huwa linafanyika pale katika ukumbi wa ikweta mtoni kwa azizi ally. 

Siku kadhaa zilizopita mkurugenzi wa G5 Modern Taarabu Hamisi Slim alijinasibu kwamba amemchukua Zungu ili kuimalisha kikosi chake, lakini leo Zungu hayupo tena. 
Hao ndio wasanii wa Taarabu...!.

0 comments:

Post a Comment