TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, October 7, 2013

TETESI: 5 STARS MODERN TAARABU, KUBADILISHWA JINA.

Baadhi ya wasanii wa 5Stars.
Bendi ya 5 stars Modern Taarabu inasemekana viongozi wake wapo mbioni kubadili jina la bendi hiyo ili kwenda na wakati. 

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake kiongozi mmoja wapo wa bendi hiyo alisema Jina hilo la 5 Stars limekuwa kama lina mikosi kwani bendi imekuwa haipandi ukizingatia mkurugenzi amewekeza pesa nyingi sana kwa kununua wasanii wenye majina makubwa katika tasnia ya taarabu lakini hakuna jipya. 

Jina jipya la bendi hiyo bado halijapatikana na hata kamati ya kuteua jina mbadala haijakaa, pia kuna wasanii watapunguzwa kazi, alisema.

0 comments:

Post a Comment