TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, October 3, 2013

T MOTTO YAPAGAWISHA BILA JOKHA KASIM...

Baadhi ya Waimbaji wa Bendi ya T MOTO.
 Bendi ya T MOTTO Modern Taarabu, siku ya J4 ilifanya show ya nguvu katika ukumbi wa Kapakabana Mwananyamala.

Bendi hiyo ambayo ilikaa muda mrefu bila kufanya show, ilikonga nyoyo za wapenzi wake kwa vibao vyao maridadi kama Domo la udaku, Behind the scene na Mwanamke hashuo, wadau walisikika wakisema kwamba wanaitaka bendi hiyo kufanya show kila J4 kama ilivyokuwa zamani.

Jokha Kassim, Muimbaji Nyota wa T MOTO.
Dosari iliyojitokeza katika show hiyo ni kutoonekana kwa Star wa bendi hiyo Jokha Kasim na pia kuonekana kwa sura ngeni nyingi za waimbaji wa bendi tofauti ambao walikuja kutoa msaada kwa bendi hiyo.

Kulikuwa na waimbaji watatu wa G5 na mpiga gitaa la solo mmoja wa bendi ya Kings Modern Taarabu anaitwa "silver mundele".

Mtandao huu uliweza kushuhudia Show hiyo iliyokuwa nzuri na ya kuvutia, T Moto mjipange vyema kwa kufanya show kama wapenzi wenu wanavyowaomba.

0 comments:

Post a Comment