TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, October 11, 2013

HASSAN VOCHA NA HASNA MASAUTI WAGOMA G5 MODERN TAARABU...

Hassan Vocha.
Wasanii chipukizi wanaokuja kwa kasi ya ajabu katika tasnia ya taarabu Hassan Vocha na Hasna Masauti wamegoma kuendelea kuitumikia bendi ya G5 kwa kile kinachosemekana ahadi hewa ambazo wamekuwa wakiahidiwa na mkurugenzi wao Hamisi Slim. 
Hasna Masauti.
Chanzo chetu cha habari kilichopo ndani ya kundi hilo la G5 kilisema kwamba hawa watoto tokea waje hapa toka kwa mkubwa Fellah wamekuwa wakizungushwa kupewa pesa zao jambo lililopelekea Hassan Vocha kutaka kuikimbia bendi hii na kujiunga na Kings lakini juhudi za Adam Mlamali kumshawishi zilimrudisha tena kundini, lakini kilichofanyika baada ya kurudi tena katika bendi ni zile zile ahadi hewa zisizotimilika! "Unajua mkurugenzi wetu asipokuwa makini bendi haitofanikiwa itakuwa kila siku tunarudi nyuma badala ya kusonga mbele, hawa watoto hawajaja katika show kibao mpaka sasa jambo linalopelekea mashabiki na wapenzi wao kuwaulizia kila tunapokwenda kupiga show!", 

Juhudi za kumtafuta kwa simu mkurugenzi wa G5 ziligonga mwamba kwani simu yake ilikuwa haipatikani hewani. Pia tulipo mtafuta Hassan Vocha ili kuthibitisha hili simu yake ilikuwa inaita bila majibu yoyote, tunawaahidi wasomaji wetu tutafuatilia zaidi.

0 comments:

Post a Comment