TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, October 2, 2013

BENDI 3 ZAMNYEMELEA NYAWANA MALKIA WA KINYAMWEZI.

Nyawana Fundikira (Malkia wa Kinyamwezi).
 Ni baada ya kutoka na "Shetani kataja Jina" na kutamba sana katika vituo mbalimbali vya radio imewafanya mabosi wa bendi tatu tofauti hapa Nchini wamtafute Nyawana.

Anaitwa Malkia Wakinyamwezi kutokana na manjonjo yake pindi anapokuwa stejini, Huyu ni Nyawana Fundikira mtoto wa mzee Isale, Wimbo wake mpya wa Shetani Kataja Jina umemfanya awe gumzo mjini na kupelekea bendi 3 kubwa za taarabu hapa nchini kumuwania ili afanye kazi katika moja ya bendi hizo. 

Akizungumza na mtandao huu Nyawana alikili kuwepo na mipango hiyo ila amesema ni mapema mno kuzitaja bendi hizo kwani bado wapo katika mazungumzo na mambo yatakapokuwa mazuri basi mashabiki zake watajua ni bendi ipi mojawapo atakuwepo

0 comments:

Post a Comment