TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, October 5, 2013

SUPERSHINE MODERN TAARABU, SIKU YA IDD-EL-HAJJI, KUTOA BURUDANI MAX BAR ILALA BUNGONI

Bendi ya Supershine Modern Taarabu yenye makazi yake Magomeni jijini Dar, siku ya idd el haji wanatarajia kufanya show ya nguvu katika ukumbi wao wa nyumbani wa MAX BAR ILALA. 

Akizungumza na mtandao huu meneja wa bendi hiyo Kais Mussa Kais alisema siku hiyo kutakuwa na burudani nyingi ndani ya ukumbi huo kwani wapo katika mazungumzo ya mwisho mwisho kuwaleta Baikoko na msaani mmoja mkubwa wa taarabu ambae atasindikiza show hiyo maalum ya Idd el haji. 

Supershine ndio habari ya mjini kwa sasa, kwani wanatamba na nyimbo zao mpya na siku hiyo wataimba nyimbo zote za zamani na watamalizia na nyimbo zao zote mpya walizoziachia hivi karibuni.

Wakazi wote wa Jijini mnakaribishwa kuja kupata burudani nzuri kabisa ndani MAX BAR ILALA BUNGONI.

0 comments:

Post a Comment