TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, October 2, 2013

MWANZILISHI WA TARADANCE, SAKATA LA THABIT ABDUL NA ALLY STAR LAENDELEA...

Ally Hemed "Star" a.k.a. Sharo Babu.
 Maelezo ya Ally star: 

Kuna mtu kamuingiza Abdallah Issa katika Malumbano yangu na Thabit Abdul
NATAKA KUMKUMBUSHA BIMA MODERN TAARAB Bend ambayo, Ally Star Sharobabu ni Mmoja kati ya Waasisi; Bend hiyo ilianzishwa 1985; BAADAE; 1987 Ikaanzishwa Bend ya MAMESH MODERN TAARAB; "KUFIKIA; 1988 Ikaja; ALL STAR MODERN TAARAB; "Baada ya miaka mi4 kufikia 1992 Ikaanzishwa; TANZANIA ONE THEATRE . BAADAE 1993 Ikazaliwa THE EAST AFRIKA MELODY; 94/95 Ikazaliwa DUMBAK MASTER'S chini ya Abdallah Issa Baada ya kuachana na Melody; Ingawa Abdallah Issa ameanza kuimba zamani, mwanangu Thabit Abdul "NAZI HAISHINDANI NA JIWE".

Kwa sasa mimi Sitafuti Umaarufu Mimi tayari maarufu kabla wewe hujaanza Chekechea, hakuna asiejua hilo, Nataka Utambue hivyo 2.

Mie siendi media kama unavyohaha wewe. Media wanataka kujua mambo toka kwangu
lakini kama unavyodai kua Media zote zinajua kama wewe ndio muasisi wa Taradance! hizo ni juhudi zako za kuhaha na Media lakini unatakiwa UNISHUKURU MIMI kwa kukuanzishia Taradance kama unabisha!
Nataka uweke wazi jambo hili:. "Nyimbo ya RUDI iliyo katika mtindo wa RHUMBA ambayo ni utunzi wa ALLY STAR SHAROBABU, na ukaimbwa na Ally Star; Na wewe Thabit Umeshiriki kupiga kinanda, wakati huo wewe Thabit Ukiwa na Bend ya TOT Taarabu ni kabla hamjaanzisha MASHAUZI. Je!, wimbo huo wa RUDI sio Taradance? 

Kosa langu kutokutangaza? HAYA NIMEKUBALI UMESHINDA WEWE KAMA KUANZISHA UMEANZISHA WEWE, SIONI FAIDA YA MABISHANO HAYA KILA LA KHERI. 

Huo ni walaka mzito ulioandikwa na ALLY STAR na kutumwa katika ofisi za taarabuzetu.blogspot.com, akijibu tuhuma toka kwa Thabit Abdul ambae alinukuliwa na mtandao huu akisema Ally Star si lolote si chochote na ameishiwa, sisi kama mtandao makini, sakata hili tunalirudisha kwenu wasomaji wetu mnaoujua ukweli mtoe maoni yenu ni nani yupo sahihi kati yao?.

0 comments:

Post a Comment