TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, October 25, 2013

HASSAN VOCHA NA HASNA MASAUTI, WAIBUKIA SUPERSHINE.

Hassan Vocha na Hasna Masauti
Waimbaji nyota wa bendi ya G5 Modern Taarabu ambao wapo katika mgomo wa kimaslahi kwa sasa, Hassan Vocha na Hasna Masauti wameibukia Supershine Modern Taarab. 

Waimbaji hawa nyota jana walionekana ndani ya Lango la jiji Magomeni katika show ya Supershine Modern Taarabu na kuimba nyimbo 2. Hasna Masauti akiimba "Huliwezi Bifu" na Hassan Vocha yeye akiimba "Mazoea Yanatabu" jambo lilillotafsiriwa na wapenzi kama ni dongo kwa Boss wao kwa kile wanachodai waimbaji hao. 

Alisikika kiongozi mmoja wa Supershine akisema atafanya mazungumzo haraka na vijana hao ili kujua kama wana mkataba pale G5 au hawana ili waweze kuwachukua kuongeza nguvu katika kikosi chao.

0 comments:

Post a Comment