TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, October 7, 2013

ASHURA MACHUPA:- NZI WA KIJANI ILIFUTWA MAKUSUDI STUDIO..!

Ashura Machupa wa Fungakazi Modern Taarabu.
 Nzi wa kijani ni wimbo ambao kwa sasa ndio umekuwa habari ya mjini kulingana na vijembe vilivyomo katika wimbo huo, muimbaji wa wimbo huo ni Ashura Machupa kutoka katika bendi ya Fungakazi Modern Taarabu, ambae naweza kusema ameutendea haki wimbo huo, kwani amejua haswa kuichezea sauti yake katika Nzi wa kijani. 

Mapema Jana wakati anahojiwa na mtangazaji MWANAISHA SULEIMAN wa redio 5 Arusha katika kipindi cha taarabu, Ashura alisema wimbo huo wa Nzi Wa Kijani mara ya kwanza ulirekodiwa katika studio moja huko Sinza lakini kwa njama za wajanja wakafanikiwa kuufuta, lakini sisi tulihama na kurekodi kwingine.

0 comments:

Post a Comment