TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Sunday, October 20, 2013

NASSORO HUSSEIN CHOLLO NAE ATIMKIA MUSCAT..



Lile wimbi la wasanii wa taarabu kwenda Muscat kufanya shughuli za muziki limeendelea kushamili baada ya muimbaji wa Zanzibar One na T Motto Nassoro Hussein maarufu kama "Chollo" nae kuelekea huko. 

Chollo ambae alipokuwa Zanzibar One aliimba wimbo uitwao "Nastaleheshwa" na alipokuwa T Motto aliimba wimbo uitwao "Wewe sio daktari wa mapenzi". 

Kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na wimbi zito la wasanii wa taarabu kuondoka nchini na kwenda Oman kufanya shughuli za muziki wa Hotel, wiki mbili zilizopita Mgeni Kisoda na Amour Salehe "Zungu" nao walipanda ndege kuelekea huko pia.

0 comments:

Post a Comment