TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, October 29, 2013

YUSUPH TEGO AITOSA 5 STARS NA KUTIMKIA MUSCAT..

Mpiga kinanda namba mbili wa bendi ya 5 Stars Modern Taarabu Yusuph Tego ametimkia Muscat kufanya muziki wa Hotel pasipo kupata ruhusa ya uongozi wake wa 5 Stars. 

Mwandishi wa habari hizi alimtafuta kwa simu mkurugenzi mkuu wa 5 Stars Mr Shark's ambae alisema Yusuph Tego ameomba ruhusa ya mwezi mmoja katika bendi hiyo na amesema kuwa anaenda kwao mara moja kusalimia, sisi kama uongozi hatuna taarifa za yeye kwenda Muscat ila nitafuatilia kwa karibu. 

Taarabu Zetu ilipopiga simu ya Yusuph haikupatikana kwa siku tatu mfululizo khali inayoonekana yupo mbali. 
Hawa ndio wasanii..

0 comments:

Post a Comment