TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, October 14, 2013

Kwenye Azimio la Arusha, Mwalimu Nyerere alisema haya kuhusu Wanawake:

"Ingefaa kuwauliza wakulima wetu, hasa wanaume, ni saa ngapi za juma na majuma mangapi kwa mwaka wanafanya kazi. Wengi hawafanyi kazi hata kwa nusu ya saa ambazo mpokea mshahara anafanya. Ukweli ni kuwa kwenye vijiji wanawake wanafanya kazi ngumu sana. Nyakati nyingine wanafanya kazi kwa saa 12 au 14 kwa siku. Wanafanya kazi hata siku za Jumapili na za sikukuu. Wanawake wanaoishi vijijini wanafanya kazi ngumu kuliko mtu mwingine yeyote Tanzania. Lakini wanaume wanaoishi vijijini (na baadhi ya wanawake mijini) wako likizo kwa nusu ya maisha yao. Nguvu ya mamilioni ya wanaume kwenye vijiji na maelfu ya wanawake mijini ambazo kwa sasa zinapotezwa kwenye udaku, dansi na kunywa, ni hazina kubwa ya nchi ambayo inaweza kuchangia maendeleo ya nchi yetu zaidi ya ambavyo tunaweza kupata kutoka mataifa tajiri."

Takwimu za sasa zinaonyesha, wakulima wadogo wanawake wanazalisha takribani asilimia sitini (60%) ya chakula chote tunachotumia, lakini ni asilimia moja (1%) tu ndio wanaomiliki ardhi.

Unamuenzi vipi Baba wa Taifa..??

0 comments:

Post a Comment