TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, October 9, 2013

MOSI SULEIMAN AGEUKIA BONGO FLEVA...!!

Mosi Suleiman.
Muimbaji wa Taarabu ambae kwa mara ya mwisho alikuwa katika bendi ya 5 Star's Modern Taarabu, Mosi Suleiman amegeukia upande wa pili kwa kutoa wimbo wa bongo fleva uitwao MAZOEA YANA TABU. 

Akizungumza na mtandao huu wa taarabuzetu.blogspot.com Mosi alisema nimeamua kuimba miondoko hii ya bongo fleva ili kuwadhihirishia wapenzi kwamba hata sisi wa Taarabu tunao uwezo mkubwa sana wa kuimba miondoko hii ya bongo fleva. 

Mosi amewaomba wapenzi wa muziki huo kumpokea na kumpa sapoti kubwa. 

Kabla ya kuwa na bendi ya 5 stars Mosi aliwahi kuimbia bendi kadhaa ikiwemo Victoria, T Motto na nyinginezo.

0 comments:

Post a Comment