TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, September 26, 2013

5 STAR'S WAELEKEA LINDI NA MTWARA BILA ALLY J WALA RAJABU KONDO!..

Baadhi ya wasanii wa 5Stars Modern Taarabu.
 Bendi ya 5 Stars Modern Taarabu imeanza ziara yake mikoa ya kusini pasipo na wasanii wake wawili mahiri ambao ni Ally J na Rajabu Kondo. 

Bendi hiyo ambayo imeondoka hapa jijini Dar kuelekea huko mikoani, jana wamefanya show ya nguvu Ruangwa, leo Nachingwea, kesho Masasi, Jumamosi watakuwa Mtwara, Jumapili watawapa raha wakazi wa Lindi mjini, na kumalizia siku ya Jumatatu pande za Mafia kwa mkurugenzi wao Shark's the Don!. 

Wanatarajia kurudi Dar wiki ijayo. Taarifa zinasema kwamba bendi inaendelea vizuri kutoa burudani kwa wakazi wa kusini.

0 comments:

Post a Comment