TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, September 19, 2013

JOKHA KASSIM AGEUKIA FILAM, AJA NA "MY FAULT".


"HII HAPA NI TRAILER TU YA FILAM YENYEWE":-

Mwimbaji mahili na wakutegemea katika tasnia ya Taarabu nchini Jokha Kassim wa T MOTO Modern Taarabu amegeukia katika uigizaji wa filam na anakuja na filamu inayoitwa "My Fault".

Akizungumza na mtandao huu Jokha alisema uigizaji ni kati ya vipaji vyake alivyojaaliwa na mwenyezi Mungu, na katika filamu hii wadau ndo watasema kama atakuwa anafaa kuimba Taarabu au Kucheza Filam.

Katika filamu hii kuna wasanii wengi wakongwe na wenye vipaji kama:-
Mzee Masinde
Muhogo Mchungu
M-2
Rakheem David
Mayugwa
Hassan Ally na mwenyewe Jokha Kassim.

Filam ipo mbioni kutoka wadau mkae mkao wa kula kumshuhudia Jokha akifanya vitu vyake katika muonekano mwingine.

0 comments:

Post a Comment