TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Monday, September 16, 2013

MANYANYASO, WIZI NA UZALILISHAJI KWA MASHAUZI CLASSIC...

Poster Feki iliyochongwa na tepeli huyo.
Siku yaIjumaa Tarehe 13/09/2013 waligundua Wizi, Unyanyasaji na Uzalilishaji wakati walipokuwa wameenda kufanya show maeneo ya Mbezi.

Blog Hii ilipata taalifakupitia kwa page ya Facebook ya "Mkurugenzi wa Mashauzi Classic" Isha Mashauzi, taarifa hiyo ilisomeka hivi:-
"Hii ndio Hali halisi ya manyanyaso niyapatayo ila namuachia mola yy ndo ano jua anisaidie hili duh kwel hii Haki".

Mwandishi wa Taarab Zetu baada ya kuisoma hiyo ikambidi aanze kudodosa na kufuatilia ni nini tatizo!?

Mkurugenzi wa Mashauzi C Mashauzilassic, Isha Mashauzi.
Tulichukuliwa na Promota .... (Jina tunalo) kwenda kupigashow siku ya Ijumaa tarehe 13/09/2013 katika Ukumbi wa La Villa Chika maeneo ya Mbezi, kilichonishangaza na kunisikitisha sana ni kitendocha kukuta Matangazo ya Mashauzi Classic (Posters) yakiwa na mchanganyiko wa wasanii tofauti, Waimbaji wa Jahazi na wacheza show wa iliyokuwa Victoria Sound, mtu huyo ambaye jina lake tunalo inasemekana ndo tabia yake ya kuandaa matamasha hewa, yeye hukutana na boss mwenye Ukumbi na kuongea naye habari za Tamasha akimweleza wasanii atakaowaleta namwisho wa siku huafikiananajamaa kuchua pesa za Show anaenda kutengeneza Posters feki kama hizi na kuzibandika kumridhisha Boss kisha yeye huingia mitini.

Siku ya tukia Mashauzi ilibidi wapige show tu kwakutokuwaangisha mashabiki wake lakini Tapeli huyo alikuwa tiyari kafanya mamboyake.

Mashauzi alipoulizwa atachukua hatua gani kwakitendo hicho alichofanyiwa alisema:- "Mimi kwakweli huwa sina matatizo na mtu ila kwa hili namuachia Mungu tu maana yeye ndo anajua yote, hata hivyo nitakutana na washauri wangu nione wanasemaji, kwasababu mtu mwenyewe tunamjua...".

taarabuzetu.blogspot.com imesikitishwa sana kwa kitendo hichi kilichofanywa kwa Mashauzi, si tunashauri huyo mtu afikishwe kwenye vyombo vinavyohusika ili aweze kuchukuliwa hatu, maana anavyobaki vile bila kuchukuliwa hatua yoyote anazoea na kuendelea na tabia yake hiyo chafu.

Mwisho tunatoa pole sana kwa kundi zima la Mashauzi Classic.

0 comments:

Post a Comment