TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, September 14, 2013

BAADA YA KUTOKA NZI WA KIJANI *KAPTENI TEMBA ATUMIWA SMS ZA KUTISHIWA MAISHA YAKE *...

Kepteni Temba, Mkurugenzi wa Fungakazi Modern Taarabu.
 Kwa mara ya kwanza tulipo ripoti kwamba Kapteni Temba yupo studio kuurekodi wimbo wake uitwao "Nzi Wa Kijani" na ni DONGO kwa mtu mmoja maarufu sana hapa jijini Dar es Salaam, baadhi ya mitandao ilianza kubeza habari hiyo na kusema haina ukweli wowote, lakini baada ya kupita siku kadhaa tulilipoti kupotea kimaajabu wimbo huo studio wakati ulisharekodiwa tayari. 

Baada ya wimbo kupotelea kusikujulikana Temba hakuishia hapo alihama studio na kwenda kurekodi kwa mara ya pili katika Studio ya Soundcrafters Temeke.

Sasa sekeseke likaanza baada tu ya kutoka kwa wimbo huo studio na kuanza kusikika redioni. Mkurugenzi wa Funga Kazi Modern Taarabu bwana Kapteni Temba amekuwa akipata sms za vitisho na watu wasiojulikana wakimtumia sms katika simu yake jambo lililomlazimu kubadili line ya simu yake.

Watu hao waliendelea kuwatumia sms hata watangazaji ambao wamekuwa wakiupiga wimbo huo au wameonekana kama kushabikia kwa namna moja ama nyingine na wao wamekuwa wakitumiwa sms za vitisho wakiambiwa waache kucheza wimbo huo. 

Pia baadhi ya wadau wa taarabu nao wamekuwa wakitumiwa sms hizo za vitisho toka kwa mtu asiejulikana wakiaswa kuacha kushabikia mambo yasiyowahusu.

Kepteni Temba baada ya kuona hali inaendelea vile akaamua kwenda kuripoti polisi vitisho hivyo.

1 comments:

Unknown said...

Mungu atawashinda na shari zao..funga kazi level nyengine wasokubali wajinyonge kwa big G.

Post a Comment