TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, September 17, 2013

SUPERSHINE KUADHIMISHA BIRTHDAY YA BENDI JUMATANO HII PALE MAX HALL ILALA BUNGONI

Baadhi ya wasanii wa Supershine Modern Taarabu.
 Bendi ya Supershine Modern Taarabu wana Rusha roho usitoe roho! kesho jumatano tarehe 18 wanatarajia kufanya sherehe ya birthday ya bendi katika ukumbi wa MAX HALL ilala Bungoni Dar!. 

Akizungumza na mtandao wa Taarabu Zetu meneja wa bendi hiyo Kais Mussa Kais alisema siku hiyo kutakuwa na keki 3 ambazo ni ya wasanii wa bendi, Wadau na Wapenzi wa Supershine na keki ya mwisho itakuwa maalum kwa wasanii ambao waliwahi kupitia Supershine kipindi cha nyuma.

Alikitaja kiingilio siku hiyo kuwa Wanaume Shilingi 4,000/= na Wanawake Shilingi 2,000/=, show itaanza saa 3 usiku.

Blog hii pia imepewa MWALIKO MAALUMU... Tutakuwepo na wote mnakaribishwa.

0 comments:

Post a Comment