TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, September 26, 2013

DAR MODERN TAARABU YAPOROMOKA KIWANGO...

Baadhi ya wasanii wa Dar Modern.
Bendi ya Dar Modern Taarabu ya jijini Dar es Salaam imekimbiwa na mashabiki katika maonesho yake, kwa sasa imebaki na show moja tu kwa wiki ambayo inafanyika katika ukumbi wa LANGO LA JIJI Magomeni Mikumi kila jumatano. 

Ukienda kuhudhulia tamasha hilo ajabu ni kwamba watu ambao wanaingia katika show zao ukiwahesabu kwa idadi hawafiki hata 15!.

Bendi hiyo ambayo hapo nyuma iliwahi kutamba na kibao chake maarufu PEMBE LA NG'OMBE imekosa mvuto baada ya kuondokewa na wasanii wake kadhaa wakiwemo Hammer Q, Salha, Mlidu Ally, Mape Kibwana, Hashim Said na wengineo wengi. 

Tunapenda kumshauri Mkurugenzi wake kuzinduka sasa na ajipange ili kuweza kuiinue Bendi na kuifufua, ajue anakoelekea sasa ni kugumu zaidi.

0 comments:

Post a Comment