TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, September 10, 2013

COAST MODERN TAARABU NA T MOTTO SHOW MNAFANYA KUMBI GANI....!?

Omary Tego wa Cost Modern Taarabu.
Wapenzi na mashabiki wa bendi za T MOTTO na COAST MODERN TAARABU kwa nyakati tofauti wamekuwa wakipiga simu katika ofisi zetu kuulizia ni kumbi zipi za burudani ambapo zinapiga show bendi hizo mbili.
Baadhi ya wasanii wa Kundi la Muziki wa Taarabu la Tanzania Moto Modern Taarabu (T-Moto), wakiwa katika Studio.
Jamali masudi mkazi wa Yombo Buza alisema yeye ni shabiki mkubwa wa T MOTTO lakini amekuwa hajui ni kumbi gani wanapiga bendi hiyo hapa Dar ili akapate burudani live. 

Pia Leyla Kasim wa Tegeta Dar alipiga simu akiomba mtandao huu uulizie kwanini Omary Tego na bendi yake hawatangazi ratiba zao au hawana show yoyote?.

Mtandao wa taarabuzetu tunawaahidi wasomaji wetukuwa tutafuatilia na tutawapa majibu pindi tutakapowasiliana na mabos wa bendi husika.

0 comments:

Post a Comment