TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Thursday, September 26, 2013

SAIDA MASHAUZI AACHIKA NDOANI...

Saida Mashauzi.
Muimbaji wa Mashauzi Classic Saida Mashauzi ameachika ndoani baada ya kukaa na mumewe miezi minne tu. 

Akizungumza na mtangazaji wa times fm Dida leo hii alhamisi, dada wa msanii huyo Isha Mashauzi amethibitisha hilo kwamba mdogo wake huyo ameachika katika ndoa hiyo na sababu kubwa ya kuachana kwao ni kwamba mume hakuwa anataka mkewe aendelee kuimba tena taarabu jambo ambalo lilipata upinzani mkubwa toka kwa Saida mwenyewe na kukataa kuacha kuimba. 

Saida Mashauzi ni msanii anaekuja kwa kasi kwa sana kwa sasa, Isha Mashauzi amesema kwamba mdogo wake huyo bado hajapewa talaka.

0 comments:

Post a Comment