TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Wednesday, September 18, 2013

MSIBA WA AHMED MGENI WASABABISHA KUGHAIRISHWA KWA SHEREHE NA SHOW YA SUPERSHINE LEO JUMATANO. TIZAMA PICHA ZA MAZISHI YA AHMED MGENI.

 Msiba mzito ulioikuta familia ya wapenda taarabu nchini kwa kuondokewa na muimbaji maarufu Ahmed Mgeni, umesababisha ile paty ya birthday pamoja na show ya leo ya bendi ya Supershine kuahirishwa mpaka pale itakapotangazwa tena. 

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu meneja na mratibu wa shughuli hiyo Kais Mussa Kais alisema Ahmed Mgeni ni mtoto wetu Supershine na hata album yake hii mpya ya SITETEREKI ameitengeneza kwetu na alikuwa anaishi kwetu wakati yupo hapa Dar, tutafanya kisomo kwa ajili yake leo saa 10 jioni.

Sote njia yetu ni moja Ahmed Mgeni umetangulia sisituko nyuma yako mungu akuondoshee adhabu ya kaburi na akupe makazi mema peponi Amen.

Inna lillah waillah rajuun pumzika kwa amani PRICE AHMED MGENI

0 comments:

Post a Comment