TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Saturday, September 28, 2013

MPIGA KINANDA MASHUHURI, AMOUR SALEH NDANI YA G5 MODERN TAARABU...


Anaitwa Saleh Amour 'Zungu.' Amefunzwa ufundi huu na Band ya siku nyingi ya All Star, pia aliwahi kuwa na Twanga Pepeta, African Theater TOT na Band nyingi, na sasa atakuwa G5 Modern Taarabu...

G5 Modern Taarab yakamilisha mipango ya kumrudisha nchini mpiga kinanda mashughuli Amour Saleh Zungu toka nchini Muscut.

Akiongea na mtandao huu Mkurugenzi wa G5 alisema bend yake sasa anaiandaa kwa kuisuka zaidi ili iwe tishio zaidi na ameamua kumchukua Zungu kwa ajili ya kuimarisha zaidi upande wa upigaji vyombo.

Wiki ijayo kuanzia tarehe 30/9 Zungu ataanza mazoezi ya nyimbo tatu atakazozitengeneza yeye mwenyewe na tatu nyingine ataziteneza Omari Kisila ili kukamilsha albam ya Pili ya G5 Modern Taarabu.

Pia alisema mbali ya Zungu yupo msanii mwingine mkubwa, yeye atamtaja siku za hivi karibuni baada ya kukamilisha nyimbo yake kati ya hizo sita, yeye atakuwa ni "Surprise" kwa wapenzi wetu hivyo wasikae mbali.

Mkurugenzi Mr Slim alisema nyimba zitakuwa ni kali sana kutokana na jinsi walivyozipangilia na zitakuwa na radha tofauti tofauti kwasababu kila nyimbo itakuwa na muimbaji wake.

Show maalumu itafanyika kwa kuwatambulisha wasanii hao wapya baada ya kukamilisha nyimbo zao,

Mr Slim pia alisema wiki ijayo wataiachia Video ya nyimbo yao mpya "DONT BREAK MY HEART" ya  HASAN VOCHA.

Wapenzi wote wa G5 Modern Taarabu mambo mazuri ndo hayo...

0 comments:

Post a Comment