TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Friday, September 20, 2013

WAIMBAJI WA TAARABU NCHINI PUNGUZENI KUJISIKIA...

 Blog hii ya taarabuzetu.blogspot.com tumepata malalamiko toka kwa watu mbalimbali wapenzi na wadau wa Taarabu Nchini kuwa, "Waimbaji wa Taarabu wanajisikia sana".

Imekuwa ni desturi kama sio tabia iliyoota mizizi kwa wasanii wa taarabu nchini Tanzania kuchelewa kufika katika show na wengine hudiriki hata kukataa kupiga picha na shabiki wake ambae amelipa pesa kuingia katika hiyo show yake. 

Leo nisingependa kuwataja wasanii husika ila wengi wao ni wale wenye majina makubwa katika tasnia hii ya taarabu nchini. 

Utakuta wameandika show inaanza saa 3 usiku lakini ajabu mpaka saa tano za usiku show haijaanza, kwanini mnakuwa mna malingo kiasi hicho? kumbukeni kuwa ninyi bila ya mashabiki hamuwezi kuthaminika! malingo sio uungwana tubadirike jamani na viongozi ni vyema mkizingatia hili ili kuwaridhisha mashabiki kupata walichokifuata.

0 comments:

Post a Comment