TANGAZA NASI

Kiatu Media

Feedjit

Tuesday, September 10, 2013

HII NI SUPERSHINE MPYA MASHABIKI WATUPOKEE...

Kais Mussa Kais, Meneja wa Supershine Modern Taarabu.
Meneja wa bendi ya Supershine Taarabu Kais Mussa Kais, amewaomba wadau na wapenzi wa taarabu nchini kuwapokea na kuwapa sapoti kubwa ili waweze kufikia malengo. 

Ameyasema hayo wakati alipokuwa akifanya mahojiano na redio 5 ya Arusha katika kipindi cha taarabu na mtangazaji Mwanaisha Suleiman. 

Kais alisema amekuja kuleta mapinduzi makubwa katika tasnia hii ya muziki wa mwambao haswa ndani ya bendi yake ya Supershine, Kais kabla ya kuwa meneja wa Supershine amewahi kuwa meneja wa T Motto zote za jijini Dar es Salaam. 

Kais Mussa ambaye kwa sasa ni Meneja wa Supershine pia ni mdau mkubwa wa muziki wa mwambao hapa Tanzania ambapo katika juhudi zake za kuinua mziki huu ameweza kujuana na watu wengi ikiwamo wamiliki wa bendi mbalimbali za taarabu, ameahidi kufanya makubwa hasa kwa bendi yake ya Supershine ila tu anaomba ushirikiano kwa wadau.

Taarabuzetu Blog tunamtakia mafanikio mema nasi tu pamoja naye "ku-promote" muziki wa Taarabu.

0 comments:

Post a Comment